Thursday, May 12, 2016

Norwich na Newcastle zashushwa daraja EPL

Ni mara ya nne kwa Norwich kushushwa daraja kutoka EPL

Klabu ya Norwich City imeshushwa daraja kutoka Ligi ya Premia licha ya kuandikisha ushindi dhidi ya Watford.

Klabu ya Newcastle United pia imeshushwa daraja.

Ushindi wa Sunderland wa 3-0 dhidi ya Everton Jumanne uliwafikisha hadi alama 38 na kwa kuwa Norwich na Newcastle hawawezi kuwafikia, moja kwa moja klabu hizo mbili zikashushwa daraja.
Kwa sasa Norwich wana alama 34 sawa na Newcastle. Klabu nyingine iliyoshushwa daraja ni Aston Villa iliyo na alama 17 kwa sasa.

Troy Deeney alikuwa amewapa Watford uongozi mechi hiyo iliyochezewa Carrow Road lakini Norwich wakajibu kupitia bao la Nathan Redmond.

Jedwali la msimamo wa ligi ya EPL kufikia 12 Mei, 2016.
NambariKlabuMechiMabaoAlama
1Leicester373280
2Tottenham373870
3Arsenal372568
4Man City373065
5Man Utd371263
6West Ham371562
7Southampton371560
8Liverpool371359
9Chelsea37649
10Stoke37-1548
11Swansea37-1046
12Everton37144
13Watford37-1044
14Crystal Palace37-942
15West Brom37-1442
16Bournemouth37-2042
17Sunderland37-1438
18Newcastle37-2534
19Norwich37-2534
20Aston Villa37-4517

Dieumerci Mbokani aliwafungia Norwich la pili naye Craig Cathcart akawaongezea la tatu kwa kujifunga.

Odion Ighalo alikomboa bao la pili lakini Mbokani akawafungia Norwich bao la nne.

Baada ya kushushwa daraja, Norwich sasa watakuwa wakichezea tu fahari mechi yao ya mwisho dhidi ya Everton Jumapili.

Watford watajaribu kumaliza msimu vyema dhidi ya Sunderland nyumbani.
Share:

0 maoni:

Post a Comment

Copyright © A star.com All Right Reserve

CONTACT:+255713365518

FACEBOOK